Hokema blog
Sunday, 5 February 2017
TAARIFA KWA UMMA KUELEKEA KWENYE VALEINTINE MUBASHARA
Friday, 6 January 2017
Thursday, 5 January 2017
Angalia Kazi za vijana hawa walio Amua Kuanzisha Kiwanda
hawa ni KESH ALUMINIUM & WELIDING WORKS wapo TABORA
wanatengeneza
VITANDA VYA CHUMA
MAKABATI YA NGUO
MEZA ZA TV
DRESSING TABLE
Waweka vioo kwenye salon na madirisha ya Aluminium
bei zao ni nafuu sana wanafanya kazi mpaka kwenye ofisi za serikali kama
kutengeneza double deca za wanafunzi
kuweka madirisha ya vioo na milango
wanapatikana kwa no...0659272900 ;0753688200;0625890655
Wednesday, 4 January 2017
Aje ya alikiba ya fanya kufuru
Thursday, 22 December 2016
Ajari mbaya tena Shinyanga
AJALI MKOANI SHINYANGA AMBAPO BUS LA FAHARI DAR SHY LIMEGONGANA NA RAV4 NA NOAH NYINGINE KUGONGWA. AJALI HII IMETOKEA ENEO LILELILE LILILOUA WATU 21 KWWENYE NOAH.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hii waliokuwa kwenye RAV4 walikuwa wamelewa sana ndani ya gari kuna hadi chupa za castle lite, na RAV ndio iliyohama upande wake na kwenda kuipiga bus upande wa kulia.
Tuesday, 20 December 2016
2G, 3G, 4G na 5G maana yake ni nini?
Katika sekta ya mawasiliano, ni kawaida kuwasikia wataalamu na wakati mwingine watu wa kawaida wakizungumzia kuhusu teknolojia ya 2G, 3G, 4G na 5G. Maana yake ni nini?
G kwenye tarakimu hizi inawakilisha 'Generation', yaani kizazi fulani cha teknolojia ya mawasiliano kwa kuangazia zaidi uwezo wa data kwenye simu.
Hakuna kipimo chochote kinachotumiwa kimataifa kuhusu kasi ya data ya simu.
Lakini wengi wanakubaliana kuhusu baadhi ya sifa za teknolojia hizi.
Teknolojia ya 1G, au kizazi cha kwanza cha data ya simu, ilianza kutumiwa 1991.
Teknolojia ya 2G ilianza pia kutumika katika kipindi hicho, ikiwa kama ndugu wa 1G.
Kwa 1G, ungeweza tu kupiga simu
Teknolojia hii sana ilikuwa analogu na simu za wakati huo zilikuwa kama hizi hapa chini...
Kisha 2G ikaja na uwezo wa kutuma ujumbe mfupi au arafa
Teknolojia ya 2G ambayo pia huitwa teknolojia ya SMS iliwezesha watu kutuma ujumbe mfupi.
Ungeweza pia kutuma ujumbe wenye picha, ambao uliitwa MMS (multimedia messaging service).
Na pia simu za waka.
Kupiga simu kwa video kuliwezekana 2001
3G na kasi yake ya data ya 2mbit/s (megabaiti 0.25 kila sekunde) ilianza kutumika wakati ambao simu za kwanza aina ya smartphone zilianza kuuzwa madukani.
Huduma yake ya mtandao haikuwa ya kasi sana lakini iliwezesha huduma ya mtandao kupatikana bila kutumia nyaya. Angalau ilikuwa hatua fulani.
Na watu waliweza kupiga simu za video.
Ili kufahamu kasi yake au mwendo wake wa upole ulivyokuwa, iwapo ungetaka kupakua filamu ya ucheshi ya David Brent: Life on the Road kutoka kwenye iTunes, ingekuchukua saa tano kupakua faili hiyo ya 4.26GB.
2010 teknolojia ya 4G ikaanza kutumika
Teknolojia hii ya kasi iliwezesha kuanza kupatikana kwa michezo mingi kwenye simu na ya kiwango cha juu.
Filamu ambayo ingekuchukua saa tano kuipakua kwa teknolojia ya 3G sasa inaweza ikakuchukua dakika 8 pekee kwa teknolojia ya 4G.
Utafiti: Betri zinazotumiwa katika simu zina sumu
Lakini 4G haipatikani maeneo yote, hata katika mataifa yaliyoendelea.
Afrika Mashariki, utaipata katika baadhi ya maeneo ya miji mikubwa.
5G ndiyo mwendo kasi?
Hii ndiyo ya kasi zaidi kwa sasa.
Tume ya Mawasiliano ya Ulaya inakadiria kwamba kati ya mwaka 2020 na 2030, utaweza kupakua filamu moja ya HD ya saa moja kwa sekunde sita pekee.
Simu za wakati huo nazo zitakuwa na muonekano gani? Kama hii hapa chini labda?