1. Mwanamke ni kama Shule, kamwe hauwezi hitimu.
2. Mwanamke anahitaji matunzo na kujaliwa, usipofanya hivyo unakaribisha wengine kufanya hayo.
3. Cheti chako cha ndoa yako na yeye sio "leseni ya udereva" ni "kibali cha kujifunza"
4. Inachukua muda kidogo mwanamke kukuamini, ni vigumu kumbadili akikuamini, ila ukijichanganya tu, msahau! Hawezi kukuamini tena.
5. Anaweza akawa mwiba mchungu au Malaika mwenye baraka, inategemeana na jinsi unavoishi nae.
6. Ni vigumu mwanamke kusahau vitu, hukumbuka mambo yaliyopita kirahisi na hii huwaumiza sana, jizuie usimuumize.
7. Wanawake huhitaji sana kuongea pale wanapokuwa too emotional (wakiwa wamekasirika au wameudhiwa). Wanapoona mwanaume hautaki kumsikiliza, huenda na kulia kwa marafiki zao wa karibu.
8. Wanawake wanapenda sana kuombwa msamaha! anapenda msamaha mara nyingi zaidi kuliko hata anavyompenda mwanaume wake.
9. Mwanamke anapokuwa na hasira, takribani nusu anayoyazungumza ni kinyume chake na hayamaanishi.
10. Wakati mgumu sana kwa mwanamke, ni wakati ambao yupo mbali na mwanaume anaempenda kwa dhati. Sio mbali kimwili tu. Hata kihisia pia.
Nitaendelea na TIPS za upande wa wanaume muda mwingine...msichoke na darasa!
"Love is magic when you understand our differences, and women are beautiful part of God's creation, you will enjoy if you understand her. Use your brain and ask for God's guidance!"
Siku Njema...
Tuesday, 20 December 2016
MAMBO KUMI MAGUMU YA KUFAHAMU KUHUSU WANAWAKE....
Labels:
HOKEMA ƁLOG
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment